2019

Baada ya kujifungua, baadhi ya akina mama hutoa maziwa kidogo sana kwa ajili ya watoto wao na wengine hukosa kabisa maziwa.
Hali hii huleta changamoto kubwa kwani mtoto huanza kulia sana na wakati mwingine kuishiwa maji mwilini na kuchemka.
Kitaalamu baada ya kujifungua homoni nyingi za uzazi zinapungua kisha homoni zingine kwa ajili ya uzalishaji wa maziwa kitaalamu kama prolactin hutengenezwa, sasa kuchelewa kwa kwa hatua hii kunaweza kuleta shida hii.


mambo gani unaweza kufanya kutibu tatizo hili?
usiishiwe na maji mwilini: hakikisha unakunywa maji ya kutosha angalau glass nane kwa siku ili kuongeza kiasi cha maji mwilini mwako.
kumbuka maziwa yako kwenye mfumo wa kimiminika hivyo maji mengi yanahitajika kuyatoa.
kula mlo kamili; ungeza ulaji wako wa zamani kwa zaidi kidogo, vyakula vya protini kama mayai, nyama,maziwa nay ng'ombe samaki na mboga za majani husaidia sana sana kuzalisha maziwa ya kutosha ambayo yanaweza kukidhi mahitaji ya mtoto.
tumia virutubisho; taasisi  nyingi za kiafya zinashauri matumizi ya madini ya clacium, vitamin D, Iron, na folic acid kama kiungo muhimu sana katika kumuandaa mama kuzalisha maziwa mengi na yenye virutubisho vya kutosha ndani yake.
nyonyesha mara kwa mara; hata kama maziwa ni kidogo sana jitahidi kumnyonyesha mtoto mara nyingi sana iwezekanavyo yaani mara 10 mpaka 12 ndani ya saa 24 au kila anapohitahi na hii itasaidia sana kutengeneza homoni ya oxytocin ambayo husaidia sana kutengeneza maziwa.
nyonyesha ziwa moja moja; ukimpa mtoto ziwa moja mpaka maziwa yakaaisha kabisa, taarifa hutumwa kwenye ubongo kwamba maziwa yameisha kabisa hivyo ziwa lingine litajazwa maziwa haraka wakati mtoto anamalizia kunyonya ziwa lingine.
matumizi ya dawa; wakati mwingine baadhi ya dawa hutumika hasa pale kiwango cha homoni inayohusika na maziwa inapoenekana iko chini sana na haiwezi kuongeza kiwango cha maziwa.
dawa ya dompiredone huweza kutumika kwa dozi ya 10mg kutwa mara nne na kuongeza mpaka kiwango cha mwisho cha 20mg kutwa mara nne.
Mama anaweza kupunguza dozi na kuacha kabisa kama maziwa yakipatikana, ila ikitokea maziwa yanapungua tena basi ataanza dozi na kuendelea nayo mpaka atakapomuanzishia mtoto vyakula vingine, mara nyingi baada ya miezi sita.
mwisho; wakati mwingine mama anaweza asipate nafuu pamoja nakutumia dawa zote, huenda sababu ya vyanzo vingine ambavyo vinakua nje ya matibabu kama historia ya upasuaji wa matiti na kadhalika hivyo anaweza kutumia maziwa mbadala ya lactogen au maziwa ya ng'ombe .

Kwa miaka mingi imekua ikifahamika kwamba kuosha sehemu za siri baada ya tendo la ndoa kuna zuia magonjwa ya zinaa kama kaswende, pangusa na mengine ambayo huambukizwa kwa tendo la ndoa, hii imekua ni kweli kwasababu magonjwa ya aina hiyo huhitaji muda wa kutosha kuweza kuanzisha makoloni yao sehemu za siri ili kuleta ugonjwa.
hivyo maji maji yenye ugonjwa huo yakishaoshwa yanasimamisha mfumo mzima wa kuanzisha ugonjwa husika.



Lakini hii imeonekana ni tofauti linapokuja swala la virusi vya  ukimwi kwani kuosha sehemu za siri hasa kwa wanawake na wanaume ambao hawajatahiriwa kumeonekana kuongeza maambukizi badala ya kupunguza.
Utafiti huu ulifanyika nchini Uganda ulichukua wanaume ambao hawajatahiriwa ambao wanatabia hiyo kisha kuchukua wanaume ambao hawana tabia hiyo na kuwafuatilia kwa muda Fulani( cohort studies) na majibu yakionyesha kuongezeka kwa maambukizi kwa 2.3% kwa wale wenye tabia ya kuosha uume wao muda mfupi tu baada ya tendo la ndoa.
Lakini utafiti mwingine ulifanyika nchini kenya kwa muda wa miaka kumi kwa wanawake 1270 na majibu yalionyesha kuongezeka kwa maambukizi ya ukimwi kwa asilimia 2.6% kwa wale walio osha sehemu zao za siri pale pale ukilinganisha na wale waliochelewa na kuosha baada ya dakika kumi mpaka 20.

je chanzo cha maambukizi haya ni nini?
Hakuna majibu ya uhakika wa swali hili lakini wataalamu wamekuja na ababu ambazo huenda ndio zinachangia kutokea kwa jambo hili kama ifuatavyo.
kuongeza ukali wa virusi; sehemu za siri za mwanamke zina maji maji ambayo yana tindikali ambayo kazi yake ni kuua wadudu ambao wanaingia ndani ya uke, sasa ukimwaga maji pale ile tidikali inaishiwa nguvu na kuwapa virusi wale nguvu.
kuongeza michubuko; baadhi ya watu huosha na sabuni au dawa mbalimbali,yale maumivu kidogo unayosikai baada ya kumwaga maji au kupaka sabuni ni kuongezeka kwa michubuko ambayo inatoa nafasi zaidi kwa virusi vya ukimwi kufanya mashambulizi.
kuvipa virusi uwezo wa kuishi na kusafiri; kwa kawaida virusi huishiwa nguvu au kufa pale maji maji yanayovizunguka yanapokauka, kuosha na maji na kuongeza maji maji na kuvihamisha sehemu zingine za sehemu za siri ambazo huenda zina michubuko Zaidi.
mwisho;Kwa lugha nyingine sio vizuri kuosha sehemu za siri muda mfupi tu baada ya tendo la ndoa, jipe muda wa kutosha kitandani na mtu wako kama dakika 10 au 20 ukiwa umepumzika au unafanya mambo mengine kisha unaweza kwenda kunawa.

1.1 PAIN
Pain is the most common symptom of disease. It is an unpleasant sensation or emotional experience
associated with actual or potential tissue damage. Any pain of moderate or higher intensity is
accompanied by anxiety and the urge to escape or terminate the feeling.
Diagnostic criteria
Self-report is the key to pain assessment. In non- or pre verbal children, facial expression is the most valid
indicator of pain; therefore use faces pain scale to assess severity. Pain should be assessed by:
Duration
Severity, e.g. does the patient wake up because of the pain
Site
Character, e.g. stabbing, throbbing, crushing, cramp like
Persistent or intermittent
Relieving or aggravating factors
Accompanying symptoms
Distribution of pain
In children pain can be assessed by Childs’ crying voice, posture, movement and colour
1.1.1 HEADACHE
1.1.1.1 Acute Headache
Diagnostic criteria
Secondary to fever and infection diseases
Secondary to local inflammatory cause
For further actions refer to fever, eye, ear and oral sections.
Pharmacological Treatment
A: Paracetamol oral 1g every 8 hours for at least 3 days
OR
A: Ibuprofen, oral 400mg 8 hourly for at least 3 days
Children A: Paracetamol 15 mg/kg/dose 6 hourly when required to a maximum of 4 doses per
24 hours
If there is no relief to paracetamol give:
A: Ibuprofen oral, 5-10mg/kg/dose 8 hourly
Note: Ibuprofen shall be given with food

Chronic Headache
Diagnostic criteria
Migraine
Cluster headache
Tension headache
Pharmacological Treatment:
Migraine
In acute attack give analgesics:
A: Paracetamol 1g immediately then every 4 hours; maximum dose 4g per day
2
OR
A: 
Acetylsalicylic acid 600mg 6 hourly.
AND
C: 
Metoclopramide (PO) 10mg 8 hourly.
OR
C: Metoclopramide IV 10mg 8hourly
In severe attack give:
C: Ergotamine tartrate 2mg 12 hourly. Not to be repeated at intervals less than 4 days.
For prevention purposes give
:
A: 
Propranolol 40-80mg 12 hourly
OR
A: 
Amitriptyline 10-50mg at night
Cluster and T
ension headache: Give analgesics as in acute headache (section 1.1.1)
1.1.2 CHEST PAIN
Differential diagnoses
Angina
Myocardial infections
Reflux Esophagitis
Lung infection
Pericarditis
Non-Pharmacological and Pharmacological Treatments
Treat as for main disease as indicated in specific chapters.
1.1.3 ABDOMINAL PAIN
1.1.3.1 Upper Abdominal Pain
Differential diagnoses
Pain related to eating food:
Dyspepsia
Gastritis
Pain related to eating food but persisted for more than three months
Peptic ulcers
Acute and recurrent pain in upper quadrant
Gallbladder diseases
Inflammatory bowel syndrome
Chronic pancreatitis
Diabetic autonomic neuropathy
Non-Pharmacological and Pharmacological Treatments
Treat as for main diseases
1.1 3.2 Lower Abdominal Pain
Diagnostic Criteria
Pain associated with diarrhoea or constipations
Intestinal involvement
Helminthes
Colicky pain in abdomen without diarrhoea or constipation

3
Colitis
Pain just before or during menstruation
Dysmenorrhoea
Endometriosis
Pain over lower abdomen and back associated with excessive white discharge in women
Pelvic inflammatory diseases
Pain during urination
Urinary tract infections (UTI)
Non Pharmacological and Pharmacological Treatments
Treat as for main disease as indicated in specific chapters
1.1.4 OTHER PAINS
Other pains may include:
Generalized body ache
Joint pain
Pain due to local infections
Pains due to injury
Eye pains
Ear pains
Non-Pharmacological and Pharmacological Treatments
For generalized pain give analgesics as in section 1.1.1. Advise the patient to rest and make a follow-up.
For joint, infections, injury, eye and ear pains treat as for main disease.
CAUTION: Do not use aspirin for abdominal pain or if a patient is vomiting or has nausea and do not use aspirin in children. Patients
with peptic ulcers should not be given acetic salicylic acid tablet.

Referral:
Refer patients to Regional and Tertiary care for:
Children with moderate and acute severe pain
No response to oral pain control
Uncertain diagnosis
All acute abdominal pain accompanied by vomiting and no passing of stool
Pain requiring definitive treatment for the underlying disease
Pain requiring strong opioids

Imarisha misuli ya uume wako na kupunguza tatizo la kumaliza mapema kwa kutumia mazoezi madogo tu (Improve your Penis function by doing simple exercises)


Kumaliza mapema (Premature ejaculation) wakati wa tendo la ndoa ni tatizo linalowakumba wanaume wengi hivi sasa, Ingawaje dawa za aina mbalimbali zimekua zikitumika kutibu tatizo hili imeonekana kwamba bado tatizo hili linazidi kuongezeka kila kukicha. Tatizo hili limekua likichangiwa na mambo mengi sana, ikiwemo yafuatayo;
  • Mwenendo wa maisha wa hivi sasa yaani watu wengi wanakula vyakula visivyokua na virutubisho kamili.
  • Matatizo ya kiafya ya muhusika
  • Na sababu nyinginezo nyingi
Kama nivyokwishakusema hapo mwanzo kwamba sababu za tatizo hili ziko nyingi sana, hivyo basi inatakiwa tusuruhishe swala hili kwa kutibu mzizi wa tatizo. 

Mbali na sababu za kiafya na zinginezo Mfumo wa uzazi wa mwanamume una misuli ya uume iliyoanzia eneo la mifupa ya kiuno (Pelvic bone), misuli hiyo ndiyo kiini cha tatizo hili (Kumaliza mapema). Nikupe mfano mmoja; Chukua picha ya watu wanaoinua vitu vizito, watu hawa wanaongeza ukubwa wa misuli yao kwa kufanya mazoezi ya viungo. Je, unaweza kuongeza ukubwa na ukakamavu wa misuli kwa kunywa dawa?? Lahasha ni jambo lisilowezekana, bali kwa kufanya mazoezi ya viungo.

Kwa kutumia mfano wa hapo juu nikurudishe kwenye kipengele cha misuli ya uume, Misuli ya uume haina tofauti na misuli mingine ya mwili, mfumo wake ni uleule. Tatizo la wanaume wengi kumaliza mapema inasababishwa na kusinyaa kwa misuli hiyo (Pelvic muscle). Tazama picha hapo chini inayoonyesha misuli hiyo;


Picha: Kwa hisani ya mtandao

Misuli ya uume ikiimalika Mwanaume hamalizi mapema pia anakua na uwezo wa kusimamisha vizuri uume wake na unakua kakamavu sio legevu.

JINSI YA KUITAMBUA MISULI YA UUME (PELVIC FLOOR MUSCLE)
Misuli hii ya uume (Pelvic floor muscle) ipo mwanzoni kabisa mwa shina la misuli ya uume. Namna ya kuitambua misuli hii fanya ifuatavyo;

Nikuulize swali moja kidogoUmeshawahi kubana mkojo?? Pengine upo maeneo ya hafla, darasani, ofisini, mpirani, kwenye gari ama safarini au sehemu ambayo unataka usipitwe na mada inayozungumziwa. Katika mazingira haya watu wengi wanajikuta wakibana mkojo kwa muda Fulani ili wamalizie uhondo wa mada Fulani au tukio fuani pengine yupo safarini na anajitahidi abane mkojo ili akojoe atakapofika.

Au ukiwa unakojoa maeneo Fulani yasiyo rasmi, pengine wakapita maofisa polisi ama migambo unajikuta unakatisha mkojo, Hivyo basi ile hali ya kubana au kukatisha mkojo unatumia misuli hiyo ya uume (Pelvic muscle), ndio breki ya mkojo.

Misuli hii ya uume ipo chini ya maungo ya mapaja katikati ya korodani na sehemu ya haja kubwa, mara nyingi sehemu hii ukiguswa au kutomaswa kwa kidole utaona uume unashtuka. Uuume unashtuka Zaidi ukiwa umesimama. 

Ndio maana wale watu wanaoingiliwa kinyume cha maumbile (Mashoga) wanaharibiwa misuli hii baadae mtu huyu (Shoga) anakuwa hana uwezo wa kusimamisha uume. Hivyo basi misuli hii ina kazi kubwa sana ya kuimarisha ukakamavu wa uume wako.

Hivyo basi misuli hii (Pelvic floor muscle) ndiyo inayotakiwa ifanyiwe mazoezi, sehemu hii ikiwa kakamavu uume unasimama vizuri na utaacha kumaliza mapema (Premature ejaculation).


NAMNA YA KUFANYA MAZOEZI YA MISULI YA UUME (PELVIC FLOOR MUSCLE EXERCISE/KEGEL EXERCISES)
Kama nilivyoeleza mwanzoni kwamba kiini cha mazoezi haya ni misuli ya uume, Hivyo ile hali ya kubana mkojo ndio zoezi lenyewe. Sio kwamba ubane mkojo, Lahasha inatakiwa uwe kama unabana mkojo wakati huna hamu ya kukojoa. Fanya hivyo kwa nguvu kwa sekunde 3 alafu utaachia, pia utafanya tena kwa sekunde 3, Vilevile utaachia tena afu utafanya tena. Unaweza kuendelea hadi sekunde 5, 10 na 30 kadiri utakavyokua unaweza. Fanya zoezi hili wakati wowote uupendao haijalishi uume umelala au umesimama, Pia ukifanya zoezi hili wakati uume wako umesimama itakua bora zaidi na misuri yako itakazika vizuri.

Uendelee na zoezi hilo mara nyingi kadri uwezavyo, ukizoea utaweza kufanya zoezi hili kwa muda mrefu zaidi na sehemu yoyote ukiwa unatembea, ukiwa umekaa, kwenye gari na sehemu yoyote ile. Uzuri wa zoezi hili unaweza kufanya sehemu yoyote pasipo watu kujua.


Natural Vitamins to increase Body Immunity

These 3 Natural Vitamins to increase Body Immunity

There is an old saying in English, whose Hindi translation is like, 'If you eat an apple a day, then stay away from the doctors'. This thing is quite true because apple has many elements that increase your immunity-resistant ability. If your immune system is good, then you survive from all kinds of diseases because most of the diseases in the body cause viruses and bacteria. Your immune system protects you from these bacteria and viruses. There are many such vitamins, which increase your immune system. Let's tell you who are those vitamins and what are those natural sources of vitamins.

Vitamin C

https://afyatrust.blogspot.com

Vitamin C is also called immunity booster vitamin. Vitamin C deficiency in the body increases the risk of many diseases. Vitamin C is known as bicarbonate acid, which is considered to be the best antioxidant. Glutathione contains vitamins containing substances that protects us from arterial diseases. By taking this, tissue builds in the body better, and the tissue that remains is available to connect with one another. In addition, Vitamin C prevents the destruction of cells.

Natural sources of Vitamin C

Vitamin C is rich in all citrus fruits like lemon, orange, amla, seasonal, grapes, tangrias, strawberries etc. Apart from this, vitamin C is also found in broccoli, capsicum, capsicum, spinach and oceanic diets. In a small lemon, up to 29.1 milligrams, a small orange contains about 51.1 milligrams and vitamin grams up to 445 milligrams in 100 gram pieces.

Vitamin B6

https://afyatrust.blogspot.com

Vitamin B6 also increases the body's immune system. Vitamin B6 supports biochemical reactions in the body, helping immune systemswork. Vitamin B6 is soluble in water and is beneficial in many diseases related to heart, skin and nervous system. This vitamin also provides relief from depression and lethargy. Vitamin B6 is also very important for the control of hormones in the body. Its deficiency increases the risk of diseases like many types of emotional disorders, heart diseases, kidney disease, multiple sclerosis, anemia, arthritis and influenza.

Natural sources of Vitamin B6

Most vitamins and nutrients meet us through diet. The best source of vitamin B6 is whole grains like wheat, millet, barley, corn, peas, green beans, walnuts etc. In non-vegetarian people this lack of vitamin is seen low because fish, eggs, chicken, mutton etc. are a good source of vitamin B6. Vegetarians can also find these vitamins easily with bananas, soy beans, carrots and green vegetables, besides cereals and dry fruits.

Vitamin E


Vitamins to increase Body Immunity
Vitamin E works like a powerful antioxidant, which enhances the body's ability to fight diseases and infections. Vitamin E is very important to increase the skin low and hair growth. Therefore, dietary vitamins should definitely be consumed.

Natural sources of Vitamin E

Vitamin E is found in vegetable oil. Apart from this, wheat, green greens, gram, barley, dates, rice grams, butter, cream, sugarcane, sprouted grains and fruits are found.
..............................................

MKANDA WA JESHI

Kwa takribani miongo mitatu sasa, tumeshuhudia ongezeko kubwa la mlipuko wa ugonjwa wa mkanda wa jeshi linaloendana na ongezeko la hususani ugonjwa wa UKIMWI. Hali hii imefanya baadhi ya watu kuamini kuwa, ugonjwa huu ni dalili ya wazi kabisa ya mtu kuwa na VVU, imani ambayo kwa kiasi kikubwa ina ukweli ndani yake ingawa si kwa wote wanaopatwa nao.
Mkanda wa jeshi au shingles au herpes zoster kwa majina ya kitabibu ni ugonjwa unaosababishwa na virus wa aina ya Varicella-zoster ambao pia husababisha ugonjwa wa tetekuwanga au chickenpox. Ugonjwa huu huathiri ngozi ambapo huambatana na vipele na michubuko kama ya kuungua yenye kuambatana na maumivu makali.

Visababishi

Kama tulivyokwisha tangulia kueleza hapo juu, ugonjwa huu husababishwa na virus aina ya Varicella-zoster ambao pia husababisha ugonjwa wa tetekuwanga. Baada ya mtu kupatwa na tetekuwanga, virus hawa hubaki katika hali ya kupooza/kutokuwa na madhara (dormant) katika neva fulani za mwili. Baada ya miaka kadhaa, iwapo itatokea kinga ya mwili ikashuka kwa sababu yoyote ile, virus hawa hupata tena nguvu/kuwa na madhara (active), kuibuka na kusababisha ugonjwa wa mkanda wa jeshi.

Kwa kawaida shambulio la mkanda wa jeshi hutokea mara moja maishani ingawa laweza kujirudia.

Vihatarishi

Mkanda wa jeshi unaweza kumpata mtu wa umri wowote ule ingawa watu walio katika makundi haya wapo katika hatari kubwa zaidi:
• Wenye umri wa zaidi ya miaka 60
• Mtu aliyewahi kuugua ugonjwa wa tetekuwanga kabla ya umri wa mwaka mmoja
• Watu ambao kinga yao ya mwili imepungua kwa sababu mbalimbali kama vile matumizi ya aina fulan za dawa, magonjwa kama vile maambukizi ya VVU (HIV/AIDS), saratani na utapiamlo.

Je mkanda wa jeshi unaambukizwa?

Hapana ugonjwa huu hauambukizwi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine! Lakini iwapo itatokea mtoto au mtu mzima ambaye hajawahi kupatwa na ugonjwa wa tetekuwanga maishani mwake na ambaye pia hajawahi kupata chanjo dhidi ya ugonjwa huo akakutana na mtu mwenye ugonjwa wa mkanda wa jeshi, mtoto au mtu huyo atapatwa na ugonjwa tetekuwanga na siyo mkanda wa jeshi.

Dalili

Dalili ya awali kabisa ya mkanda wa jeshi ni maumivu makali sehemu fulani/ upande mmoja wa mwili yakiambatana na hali ya ganzi na hisia za kuungua kwenye ngozi. Maumivu pamoja na hisia za kuungua huwa makali sana na hutokea kabla ya vipele/michubuko kutokea kwenye ngozi. 
Kawaida, vipele au michubuko huusisha eneo fulani la mwili kuanzia kwenye uti wa mgongo kuzunguka kuelekea eneo la tumbo au kifua. Michubuko pia inaweza kutokea kwenye maeneo yanayozunguka uso, macho, mdomo au masikio.
Dalili nyingine ni pamoja na
• Maumivu ya tumbo 
• Homa 
• Maumivu ya mwili mzima 
• Vidonda sehemu za siri 
• Maumivu ya kichwa 
• Maumivu ya viungo 
• Kuvimba kwa mitoki/ matezi 
Iwapo neva za maeneo ya uso zitaathiriwa, mgonjwa anaweza kupatwa na matatizo ya kuona, kuonja, au kusikia.

Vipimo

Ni nadra sana kufanya Vipimo maalum kwa ajili ya utambuzi wa ugonjwa huu, isipokuwa kwa nchi zilizoendelea. Kwa ujumla utambuzi wa ugonjwa huu hufanyika kwa kuchukua historia ya mgonjwa na kuchunguza sehemu ya ngozi iliyoathiriwa. 
Vipimo vya damu yaani FBP huonesha ongezeko la chembe nyeupe za damu na antibodies dhidi ya virus wa tetekuwanga.

Matibabu

Matibabu ya mkanda wa jeshi hujumuisha matumizi ya dawa kama vile Acyclovir, Famciclovir na Valacyclovir kwa ajili ya kuua virus wanaosababisha ugonwja huu. Dawa hizi husaidia kupunguza maumivu, kuzuia madhara zaidi ya ugonjwa huu na kupunguza muda wa ugonjwa.
Dawa hizi hutolewa angalau saa 72 baada ya mgonjwa kuanza kuhisi maumivu na hali ya kuungua. Ni vema dawa zianze kutumika kabla ya vipele/michubuko kujitokeza.
Jamii ya dawa za corticosteroids kama vile prednisolone husaidia kupunguza maumivu na uvimbe kwa badhi ya wagonjwa. Dawa nyingine zinazofaa kutumika ni pamoja na jamii ya antihistamines kwa ajili ya kupunguza muwasho, dawa za maumivu, calamine lotion kwa ajili ya kupunguza muwasho. Aidha mgonjwa anashauriwa kupata mapumziko ya kutosha

Matarajio

Mkanda wa jeshi kwa kawaida huchukua kati ya wiki mbili hadi tatu kupona wenyewe. Aidha ni nadra sana kwa ugonjwa huu kujirudia tena. Iwapo neva zinazothibiti mwendo katika mwili zitakuwa zimeathirika, mgonjwa anaweza kupatwa na kupooza kwa muda au kwa kudumu kwa sehemu ya mwili iliyoathiriwa. Wakati mwingine, maumivu yanayosababishwa na mkanda wa jeshi yanaweza kudumu kwa miezi mpaka mwaka hata baada ya mgonjwa kupona kabisa. Maumivu haya yanayojulikana kama postherpetic neuralgia kwa kawaida huwakumba wagonjwa wenye umri wa zaidi ya miaka 60 na husababishwa na uharibifu katika neva za mwili.

Madhara

Madhara ya mkanda wa jeshi ni pamoja na kupatwa na shambulio jingine la ugonjwa huu, maambukizi ya bakteria, upofu iwapo eneo la jicho litahusika, ukiziwi, maambukizi katika utando wa ubongo (encephalitis), uwepo wa vimelea kwenye damu (sepsis) au ugonjwa unaoitwa Ramsay Hunt Syndrome iwapo utahusisha neva za uso.

Kinga

Epuka kabisa kugusa eneo lenye vipele au michubuko kwa mtu mwenye mkanda wa jeshi au tetekuwanga iwapo hujawahi kuugua au kupata chanjo ya tetekuwanga. 
Ni vema kupata chanjo dhidi ya virus wa Varicella zoster kama inapatikana katika nchi au eneo ulilopo. Tafiti zimeonesha kuwa, watu wazima wanaopata chanjo hii wana uwezekano mdogo sana wa kupata madhara ya mkanda wa jeshi kuliko wale wasiochanjwa

Ni ugonjwa unaowaathiri sana watoto mpaka kufananishwa kuwa ni moja ya hatua za ukuaji wa mtoto. Mgonjwa wa tetekuwanga hutokewa na vijipele vyenye majimaji mwili mzima. Vijipele hivi huwa vinawasha kitendo kinachomfanya mgonjwa wa tetekuwanga kutojisikia vizuri huku akishinda anajikuna mwili mzima. Tetekuwanga husababishwa na virusi kwa kitaalamu hujulikana kama Varicella Zoster (VZV).

UGONJWA WA TETEKUWANGA

Mara nyingi ugonjwa huu wa tetekuwanga huwa haujirudii, hii ndiyo sababu imezoeleka sana kwa wengi kusema kama haujawahi kuugua basi usikae karibu na mgonjwa wa tetekuwanga. Ikumbukwe kuwa, ugonjwa wa tetekuwanga unayo kinga ingawa hapa kwetu upatikanaji wake bado haujasambaa sehemu zote.

Dalili za ugonjwa wa tetekuwanga

Dalili kuu za ugonjwa wa tetekuwanga ni vijipele (kama malengelenge) vinavyowasha. Ugonjwa huu huchukua muda mpaka kuanza kujitokeza kwa dalili zake, mgonjwa wa tetekuwanga ataanza kuona dalili hizi baada ya siku 21 tangu virusi vya ugonjwa huu kuingia kwenye mwili wake (baada ya maambukizi). Ukiachana na vijipele vinavyowashwa, dalili nyingine za ugonjwa wa tetekuwanga ni kama;
  • Kuumwa kwa kichwa
  • Homa
  • Kupungukiwa kwa hamu ya kula
Hizi ni dalili za awali ambazo huanza kujitokeza kabla ya vipele kuanza kuchomoza, mara nyingi huchukua siku moja au mbili mara baada ya kuanza kusikia dalili hizi mpaka kuanza kujitokeza kwa vijipele. Vijipele vya tetekuwanga hupitia hatua kadhaa;
  • Vijipele vyekundu au pinki hujitokeza mwili mzima
  • Vijipele huiva na kuanza kutoa majimaji
  • Vijipele vinavywea na kuanza kukauka
Kumbuka, vijipele hivi havijitokezi kwa wakati mmmoja, hivyo wakati vingine vinapona, kuna vingine vitakuwa ndiyo vinatokeza.
Mgonjwa huendelea kujisikia vibaya mpaka vijipele vikauke, na hatua hii huweza kuchukua hadi wiki mbili mpaka kupotea kabisa.

Nini husababisha Tetekuwanga?

Kama tulivyoeleza hapo juu, tetekuwanga husababishwa na virusi ambavyo kwa kitaalamu hujulikana kama Varicella Zoster (VZV). Mara nyingi ugonjwa wa tetekuwanga huambukizwa kutokana na kugusana na mtu mwenye ugonjwa wa tetekuwanga. Virusi vya tetekuwanga huendelea kuwa na uwezo wa kuambukiza mpaka malengelenge (vijipele) viwe vimetumbuka na kukauka. Hivyo epuka makutano na mgonjwa wa tetekuwanga mpaka vipele vitakapokauka kabisa. Virusi hivi huweza kuambukizwa kwa njia zifuatazo;
  • Mate
  • Kukohoa
  • Kupiga chafya
  • Kugusa majimaji ya malengelenge ya tetekuwanga

Makundi yaliyo kwenye hatari ya kupata Tetekuwanga

Watu waliowahi kuumwa au kutumia kinga za tetekuwanga ni ngumu sana kupata maambukizi ya tetekuwanga. Pia, mtoto mchanga huweza kulindwa dhidi ya maambukizi ya tetekuwanga kutokana na kinga kutoka kwa mama yake ambayo huzaliwa nayo, lakini kinga hii huendelea kudumu kwa miezi mitatu tuu.
Mtu yoyote ambaye hajawahi kuumwa tetekuwanga, yupo kwenye hatari ya kuambukizwa ugonjwa huu, lakini makundi yafuatayo yapo kwenye hatari kubwa zaidi;
  • Wanaoishi na wagonjwa wa tetekuwanga
  • Walio chini ya umri wa miaka 12
  • Wanaoishi na watoto
  • Wanaohudumia watoto kwenye vituo vya kulelea watoto au shule za watoto
  • Wenye upungufu wa kinga uliosababishwa na magonjwa au kuugua.

Uchunguzi wa Tetekuwanga

Inashauriwa uende hospitali mara moja baada ya kuona vijipele visivyoeleweka, haswa kama vijipele hivyo vitaambatana na baridi yabisi au homa.
Daktari atavichunguza vijipele, pia uchunguzi wa kimaabara utahitajika ili kuhakikisha kama ni kweli vijipele hivyo ni vya ugonjwa wa tetekuwanga.

Dalili mbaya za tetekuwanga

Nenda hospitali haraka iwezekanavyo kama utatokewa na moja ya dalili zifuatazo;
  • Vijipele vimetapakaa hadi machoni
  • Vijipele vimekuwa vyekundu sana, vinauma na vya ujoto (hii inaweza kumaanisha kuna mashambulizi ya bakteria)
  • Unajisikia kizunguzungu
  • Unapata shida kwenye kupumua
Mara nyingi makundi ambayo yapo kwenye hatari ya kupata madhara makubwa mpaka yakapelekea kutokea kwa dalili mbaya za tetekuwanga ni;
  • Watu wazima
  • Wazee
  • Watu wenye upungufu wa kinga
  • Wamama wajawazito
Ukiachana na Tetekuwanga, makundi haya, pia yapo kwenye hatari kubwa ya kuambukizwa tetekuwanga ikaambatana na maambukizi ya VZV pneumonia au bakteria wanaoshamulia ngozi, maungio na mifupa.
Endapo mama mja mzito atashambuliwa na virusi vya tetekuwanga, basi kuna uwezekano wa kujifungua mtoto mwenye matatizo kama;
  • Kutokukua vizuri
  • Kichwa kidogo
  • Matatizo ya macho

Matibabu ya Tetekuwanga

 Mara nyingi watu walioambukizwa virusi vya tetekuwanga, hushauriwa kuanza kutumia dawa zitakazowasaidia kupunguza athari za tetekuwanga kama Homa, kuwaswha nk. Kwa watoto wenye afya bora, cha muhimu ni kudhibiti dalili, kwahiyo hutumia dawa za kupaka Calamine lotion ambayo hudhibiti vipele, na dawa ya kunywa antihistamines kama Cetrizine.
Kwa wagonjwa wenye upungufu wa kinga mwilini, hupewa dawa zifuatazo interferon alpha, acyclovir. Wazazi wanashauri wasiwapeleke watoto kwenye maeneo yenye mkusanyiko kama shule, sehemu za kuchezea nk ili kuepuka kuwaambukiza wengine. Kama ni mtu mzima, inashauriwa kutotoka nje mpaka utakapopona.
Daktari atakuandikia dawa zitakazokusaidia kukabiliana na dalili za ugonjwa huu na siyo kutibu ugonjwa, bali kupunguza makali yaletwayo na tetekuwanga. Kwa kupunguza makali kutakupelekea mfumo wa kinga kupona haraka. 

Jinsi ya kujikinga na Tetekuwanga

Mwaka 1995 mamlaka ya chakula na dawa ya Marekani ilipitisha matumizi ya Chanjo kwa ajili ya ugonjwa huu kwa watoto wenye afya bora na watu wazima wenye afya bora.
Matumizi ya kinga ya tetekuwanga yanaweza kusaidia kupunguza uwezekano wa kushambuliwa na virusi vinavyosababisha ugonjwa huu. Kinga hii hutolewa kwa watoto wadogo kuanzia miezi 12 hadi 15 na baada ya miaka 4 au 6 inashauriwa kurudia ili kuimarisha nguvu Zaidi.
Kwa watu wazima ambao hawajawahi kuumbwa tetekuwanga na wala kupata kinga, wanashauriwa kuepuka kukutana na watu wanaoumwa tetekuwanga.

UGONJWA WA KICHOCHO

Ugonjwa wa kichocho, ni ugonjwa unaosababishwa na vimelea vinavyojulikana kwa kitaalamu kama schistosoma. Ugonjwa huu huathiri zaidi ya watu milioni 207 duniani na kati ya hao asilimia 85% ni katika bara la Afrika. Baada ya ugonjwa wa malaria na maambukizi ya minyoo, kichocho ni wa tatu katika magonjwa makubwa ya kitropiki.
Kichocho ni ugonjwa ambao huathiri eneo fulani la jamii au eneo fulani la kijiografia kwa kitaalamu tunaita endemic, ambapo watu wanaathirika kutokana na shughuli zao za kila siku mfano wakulima, wavuvi, na vilevile kutokana na starehe kama kuogelea kwenye bwawa lisilo salama au ziwani.

Maambukizi ya ugonjwa huu wa kichocho hutokea pale mabuu (larvae) ya vimelea vya shistosoma yalioachiwa kutoka kwa konokono wa majini yanapopenya ngozi ya mtu aliye kwenye maji yalioathiriwa.
Ndani ya mwili wa binadamu haya mabuu (larvae) huendelea kukomaa na kuwa vimelea kamili, vimelea hivi hupenda kuishi kwenye mishipa ya damu, vimelea jike hutaga mayai, ambapo baadhi ya mayai hutolewa kwa kukojoa au kwa njia ya haja kubwa. Na mzunguko huendelea.
Kuna aina ngapi za kichocho?
Kuna aina mbili za kichocho ambazo ni:
  • Kichocho cha utumbo ama intestinal schistosomiasis na
  • Kichocho cha mfumo wa mkojo ama urinary schistosomiaisis
Kila aina ya kichocho kinaletwa na aina tofauti za vimelea hawa wa schistosoma kama ifuatavyo:
  • Kichocho cha Utumbo (Intestinal schistosomiasis) husababishwa na vimelea vya Schistosoma mansoni  na Schistosoma intercalatum
  • Kichocho cha Utumbo aina ya Asia (asian intestinal schistosomiasis) husababishwa na vimelea aina ya Schistosoma japonicum na Schistosoma mekongi
  • Kichocho cha mkojo (Urinary schistosomiasis) husababishwa na vimelea jamii ya Schistosoma hematobium
Dalili za kichocho
  • Maumivu ya tumbo
  • Kuhara damu hasa kwa kichocho cha utumbo
  • Kukojoa damu (terminal hematuria) hasa kwa kichocho cha mkojo
  • Kikohozi
  • Homa
  • Uchovu
  • Ngozi kuwasha (cercarial dermatitis) kwa jina lingine swimmers itch
Vipimo na Uchunguzi
  • Kuangalia uwepo wa mayai ya vimelea kwenye mkojo na kinyesi kwa kutumia Hadubini.
  • X-ray ya tumbo
  • Ultrasound ya tumbo
  • Kipimo cha damu (complete blood count)
  • Cystoscopy kwa kichocho cha mkojo
  • Sigmoidoscopy/proctoscopy kwa kichocho cha utumbo
Matibabu
  • Kichocho hutibiwa kwa kutumia dozi ya mara moja ya dawa iitwayo Praziquantel
Madhara ya Kichocho
  • Kansa ya kibofu cha mkojo (cancer of urinary bladder)
  • Figo kushindwa kufanya kazi
  • Cor pulmonale
  • Gastrointestinal bleeding - Kuvuja damu ndani ya mwili hasa katika mfumo mzima wa chakula
  • Portal hypertension
  • Seizures - Kifafa au degedege
  • Reflex nephropathy
Jinsi ya kuzuia kichocho
  • Kuondoa na kuangamiza konokono waliopo kwenye maji au ambao hupenda kuishi kwenye maji ambao ni muhimu katika mzunguko wa kuuwaji wa vimelea vinavyoleta kichocho kwa kutumia Acrolein, copper sulfate na niclosamide.
  • Kwa sasa kuna utafiti unaendelea kwa ajili ya kutafuta chanjo ya ugonjwa huu wa kichocho.

Suggested First Foods after 6Months age

First foods can be prepared easily and cheaply at home without salt, seasonings and sweeteners. The foods should at first be mashed and smooth, but you can quickly move on to coarsely mashed foods and coarser textures. General suggestions include:
Start with a single food rather than a mixture.
Offer infant cereal first as it is fortified with iron and makes an ideal first food. Mix with expressed breast milk or formula to a smooth texture.
Otherwise, there is no particular order for foods:
Give vegetables and fruits, introduce meats, or chicken, and ‘finger foods’ such as toast..
Always sit with your baby while they are eating.
Encourage drinking water from a cup.

Malaria ni ugonjwa unaoathiri watu wengi sana duniani. Malaria husababisha vifo vya watu milioni 2.7 duniani kote, ambapo vifo vingi hutokea barani Afrika. Ugonjwa wa malaria huonekana katika nchi 100 duniani kote.

Kwa Tanzania, mikoa ambayo inaongoza kwa maambukizi ya malaria ni Kagera (41.1%), Lindi (35.5%), Mtwara (36.6%), Mwanza (31.4%), Mara (30.3%). Mikoa ambayo  maambukizi ya malaria ni kidogo  ni Manyara (1%), Kilimanjaro (1%) na Dar-es-salaam (1.2%). Kwa Zanzibar, maambukizi ya malaria ni kwa asilimia 0.8.
Malaria huonekana sana katika kanda ya Tropiki.Ugonjwa huu wa malaria uligunduliwa mwaka 1880 na Charles Louis Alphonse Laveran, katika hospitali ya jeshi ya Constatine, Algeria, baada ya kuona vimelea vya plasmodium, kutoka kwa mgonjwa aliyefariki kwa ugonjwa huo.
Malaria ni kati ya magonjwa ya maambukizi ambao husababishwa na vimelea vya Plasmodium, ambavyo humfikia binadamu kupitia kung’atwa na mmbu aina ya Anopheles jike.
  1. Plasmodium falciparum - Hupatikana sana katika nchi zilizopo katika jangwa la sahara. Asilimia 75 ya wagonjwa wote wa malaria barani Afrika husababishwa na vimelea hivi. Mwaka 2006, kati ya watu milioni 247 duniani waliougua malaria, asilimia 91 walisababishwa na vimelea hivi (Afrika 98%) na kusababisha vifo kwa asilimia 90 mwaka huo huo barani Afrika.
  2. Plasmodium malariae - Pia hupatikana katika nchi zilizopo katika jangwa la sahara, Asia ya Mashariki, Indonesia na katika visiwa vya magharibi mwa Pacific. Kati vya vimelea vyote vya malaria, plasmodium malariae ndio huonekana kwa uchache zaidi.
  3. Plasmodium ovale - Hupatikana Afrika Magharibi, Ufilipino, Mashariki mwa Indonesia, Papua New Guinea, Cambodia, Bangladesh, India, Thailand na Vietnam.
  4. Plasmodium vivax - Huonekana katika bara la Marekani, Latin Amerika na baadhi ya sehemu za bara la Afrika.
  5. Plasmodium knowlesi - Hupatikana katika bara la Asia ya mashariki katika nchi za Bormeo, Myanmar, Malaysia, Ufilipino, Singapore na Thailand. Haipatikani katika bara la Afrika.
Mwenyeji wa msingi ya vimelea vya malaria ni mbu aina ya anopheles wa kike, ambae pia ni msambazaji, na binadamu ni mwenyeji wa kati. Mbu anapokuwa anajipatia chakula kwa kunywa damu kwa kuuma binadamu mwenye maambukizi ya vimelea vya malaria, ndio mzunguko wa kwanza huanza, ambapo gametocyte za vimelea vya plasmodium hugawanyika ndani ya mbu na  kutengeneza gametocyte za kike na za kiume na baada ya hapo gametocyte hizo za kike na za kiume, hujiunga ndani ya mfumo wa chakula wa mbu na kutengeneza Ookinete ambayo hupenyeza kwenye kuta za mfumo wa chakula na kutengeneza Oocyst nje ya ukuta wa mfumo wa chakula, na hapo hupasuka na kutengeneza Sporozoites na kuhamia kwenye tezi za mate za mbu, na kuwa tayari kuambukiza binadamu mwengine pindi mbu anapojitafutia chakula.
Kwa mbu jike damu ndio lishe yake wakati dume lishe yake ni nekta ya mimea, hivyo mbu dume hasambazi ugonjwa huu. Na mbu jike aina ya anopheles hupenda kujipatia lishe kipindi cha usiku.
Maambukizi ya malaria yanaweza kupatikana kwa kuongezewa damu ingawa ni nadra sana.
Kwa Binadamu pindi anapong’atwa na mbu hupata maambukizi kupitia mate ya mbu, na vimelea vya plasmodium kwenye hatua ya sporozoites huingia kwenye damu na kuelekea kwenye ini ambapo hutengeneza schizonts na baadae schizonts hupasuka na kuachia merozoites kuelekea kwenye damu na kutengeneza immature trophozoite  kiataalamu zinajulikana kam ring stage ambapo baada ya hapa huwa kuna hatua mbili tofauti zinazofuata,hatua ya kwanza ni mature trophozoites na kutengeneza schizont nyingine kwenye damu na vilevile schizont hii hupasuka na kutoa immature trophozoites na kuendelea kujirudia tena hatua hii. Hatua nyingine ni gametocyte ambayo hubebwa na mbu.

Dalili za ugonjwa wa malaria
  • Homa
  • Maumivu ya kichwa
  • Kichefuchefu
  • Kutapika
  • Maumivu ya misuli
  • Manjano
  • Degedege
  • Kupoteza fahamu
  • Kukua kwa wengu
  • Dalili za mwanzo hutokea kati ya siku 10 hadi wiki 4, na dalili nyingi hutokea pale hatua ya merozoites inapoachiwa nyingi kwenye damu baada ya schizonts kupasuka.
Malaria ya kichwa (cerebral malaria)
  • Matatizo ya kupumua (pulmonary edema)
  • Viungo kushindwa kufanya kazi (organ failure)
  • Upungufu wa damu
  • Upungufu wa sukari mwilini (hypoglycemia)
  • Shinikizo la chini la damu (hypotension)
  • Haemoglobinuria
  • Disseminated intravascular coagulopathy
  • Metabolic acidosis
  • Kipimo cha damu na kutumia hadubini
    • Thin film--hutumika kutambua aina ya vimelea vya plasmodium (falciparum,ovale,vivax,malariae)
    • Thick film---hutumika kutambua idadi ya vimelea/µL
  • Kipimo cha damu bila kutumia hadubini
    • Malaria Rapid Diagnostic Test
  • PCR
  • Dawa za malaria
    • Mstari wa kwanza (dawa mseto)
      • Artemether plus Lumefantrine
      • Dihydroartemisinin plus Piperaquine
    • Mstari wa Pili
      • Amodiaquine
    • Mstari wa tatu
      • Quinine
  • Dawa za kushusha homa na maumivu
  • Paracetamol
Kama sehemu ya tiba, mgonjwa anashauriwa pia kula na kunywa maji ya kutosha.
  • Kuzuia mazalio ya mbu
    • Fyeka vichaka na ondoa madimbwi ya maji katika  maeneo yanayokuzunguka.
  • Kuzuia kung’atwa na mbu
    • Matumizi ya vyandarua vyenye dawa ya kuua mbu
    • Matumizi ya dawa za kupulizia za kuua mbu majumbani
    • Matumizi ya dawa za kupaka za kuua mmbu
  • Dawa za kuzuia malaria kwa wasafiri watokao nchi sizizo na malaria
    • Proguanil
    • Malarone
    • Mefloquine
  • Dawa za kuzuia malaria kwa kina mama wajawazito (IPT)
    • Sulfadoxine Pyrimethamine (SP) hutolewa kwa kina mama katika wiki ya 20 nawiki ya 36 ya ujauzito..............................................................................................

MKRdezign

{facebook#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {twitter#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {google-plus#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {youtube#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {instagram#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL}

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget