Articles by "Afya yangu"


Laxatives: Medicines producing gentle action of the bowels. Laxatives are used for non-persistent constipation. Sometimes it is given with a carminative to prevent griping.


Herbs for laxatives

Pansy Herb
Cascara Bark
Turtle Bloom Leaves
Balmony Leaves
California Barberry Root
Culvers Root
Dandelion Root
Rhubarb Root
Oregon Grape Root
Virginia Poke Root
Cape Aloe
Sacred Bark
Wahoo Bark
Alder Bark (Europ. Black)
Indian Senna Fruit
Senna Leaves
Blackthorn Flowers
Mandrake Root
May Apple Root
Buckthorn Bark
Mountain Grape
Senna Pods
Hart’s Tongue
Fringe Tree
Wormwood 

References

https://ift.tt/2Y3Z82w



 




 



Kuumwa na kichwa kumegawanyika sehemu kuu nyingi sana japo kuwa 1% yake ni ashirio la matatizo ya kiafya ambayo yame-advance. Kama vile concussion of brain,meningitis,encephaliti, na stroke. Kuumwa na kichwa pia inawezatokana na matatizo ya taya, meno au hata kula vitu vya baridi zaidi. Vyakula vyenye nitrite au monosodium glutamate.

Sehemu ambazo huuma ni kama ifuatavyo:

- Mfumo wa fahamu ambao upo kwenye fuvu la kichwa.
- Baadhi ya neva za fahamu zilizoko usoni

Misuli ya kichwani
Mishipa inayopatikana kwenye fuvu la kichwana chini ya ubongo kuna mifumo ya fahamu yenye hisia. Kumbuka fuvu na tishu za ubongo kwa zenyewe haziumi kwani hazina mifumo ya fahamu ambayo inahisia.
Mambo haya 12 nayo yanahusika sana.

1: Nervous tension headaches;
Ni maumivu ya kichwa endelevu upande mmoja au pande zote za misuli ya shingo na upande wa juu wa mgongo,kuumwa na kichwa pamoja na kusinzia. Tumia vitamin b2 na c , ounguza au acha matumizi ya sukari,kahawa,chakula chenye kukusababishia mzio,misongo ya mawazo na ufanye mazoezi yakutosha.

2: Cluster headaches;
Kichwa kuuma haswa upande mmoja wa kichwa kwa maumivu makali, machozi humtoka mtu na makamasi kwa mbali. Kitu cha kwanza ni kutumia chakula chenye protein ya kutosha, epukana na chakula chenye mzio kwako.

3: Hangover headaches;
Hii ni hali ya kichwa kuuma kwa sababu ya matumizi makubwa ya vinywaji vikali haswa pombe. Weka barafu chini ya kichwa yaani maeneo ya kichogoni au shingoni,kunywa maji mengi na juice ya matunda freshi na uache pombe.

4: Exertion headaches;
Hutokea pale ambapo mwili utatumika sana na haswa kwenye ngono. Weka barafu linalouma, kula mlo kamili na usifanye mazoezi.

5: Caffein headaches;
Hali hii hutokea pale ambapo umeacha matumizi makubwa sana ya kahawa kwa ghafla. Kunywa kiasi kidogo cha kahawa kuondoa maumivu na upunguze matumizi kidogokodogo mpaka utakapo acha kabisa.

6: Sinus headaches;
Maumivu haya huanzia upande wa kulia na kushoto wa pua na kupanda mpaka kichwani. Kula vitamini C kwa wingi na umuone mtaalamu wa afya maana saa zingine hii utkana na maambukizi.

7: Bilious headaches;
Kichwa na macho huuma haswa kipanda uso na husababishwa na kula sana, kula vibaya, kutofanya mazoezi na kukosa choo. Fanya mazoezi na kunywa maji yakutosha na kasha fanya enema.

8: Hunger headaches;
Maumivu ya kichwa ambaya husababishwa na kutokula kwa muda. Kula chochote ilimradi kiwe ni protein au carbohydrates .

9: Eyes ram headaches
Haya ni maumivu yanayotokea kwenye macho na wengi hudhani labda wameangalia vibaya japo saa zingine inaweza kuwa sababu. lakini chanzo chake haswa ni ubongo kufanya kazi kupita kiasi. Badili mtindo wa maisha na kama ni mtumiaji wa miwani ni vyema ukamuana mtaalamu aangalie kama lensi zimepotea nuru au la.

10: Menstrual headaches;
Hali hii hutokea kwa kina mama kipindi cha yai kupevuka. Hutokana na mabadiliko ya hormone, muone mtaalamu wa afya.

11: Arthritis headaches;
Haya ni maumivu ya kichwa yanayosikika mpaka shingoni na saa zingine mpaka mgongoni ambayo husababisha maumivu haswa unapozidisha mwendo au shughuli. Kitu kikubwa ni kutibu ugonjwa unaosababisha hali hiyo.

12: Hypertension headaches;
Ni maumivu ya kichwa chote, mwendo mkubwa pia huongeza maumivu. Hali hii husababishwa na shinikizo la damu. Tibu au pambana kushusha shinikizo la damu na halii itaisha bila shaka.

Kabla ya kukupa dawa na ushauri wangu nina maswali nikuulize unijibu.

Je unapata Usingizi wa kutosha? Unalala usiku masaa mangapi? Je, unakunywa maji ya kutosha? Una miaka mingapi? Unapata haja kubwa ya kutosha? Nenda pia kapime macho yako na ukapime tena kwenye mishipa yako ya fahamu huenda una matatizo. Na kitu kingine unakuwa upo juani uwe unavaa kichwani kofia.

DALILI ZA KIPANDA USO
Kipanda uso (Migraine) ni ugonjwa au maumivu makali ya kichwa anayokuwa nayo mtu baada ya mshipa wa damu (Enlargement of Artery ) kutanuka katika kichwa chake.

Baada ya kutanuka kwa mishipa hii ya damu, pia kuna kemikali ndani ya mwili zinazozalishwa na kuizunguka mishipa hii na kupelekea mtu apate maumivu makali ya kichwa na kutanuka zaidi kwa mishipa.

Maumivu makali ya kichwa hupelekea mfumo wa utendaji kazi wa mwili pia ubadilike, mtu atapatwa na kichefuchefu, kutapika, kuharisha, katika utumbo chakula hakitanyonywa vizuri kiingie mwilini, mtu atashindwa kuona vizuri maeneo yenye mwanga na kutopenda kukaa mazingira yenye sauti au kelele.

Vipo vitu mbalimbali vinavyoweza kuchangia mtu apate tatizo la kipanda uso, vitu hivi haimaanishi kuwa ni lazima kusababishe upate na hata kama haupo katika mazingira ya vitu hivi haimaanishi kuwa huwezi kupata tatizo la kipanda uso, miongoni mwa vitu hivyo ni kama vile: sauti kali au kelele, harufu kali, aleji, mwanga mkali, kuvuta sigara, matatizo ya kukosa usingizi, kukaa bila kula kwa muda mrefu, pombe, kubadilika badilika kwa siku za mwanamke (menstrual cycle fluctuations).

Inawezekana ukawa na tatizo hili la kipanda uso, miongoni mwa vitu vinavyowasaidia watu wenye kipanda uso ni kutumia dawa mbalimbali ukijumuisha dawa za maumivu zenye mchanganyiko na caffeine, pia utumiaji wa chai au kahawa umesaidia baadhi ya watu kuwapa nafuu ya maumivu makali ya kichwa.

Tunaweza kupunguza hatari (risk) ya kupata kipanda uso kwa kubadilisha staili ya maisha yetu ya kila siku, kuepuka vitu vyenye harufu kali, kuepuka utumiaji wa tumbaku (sigara), kupata muda wa kutosha kuupumzisha mwili (kulala), kufanya mazoezi, kutokaa bila kula kwa muda mrefu, kunywa maji ya kutosha.Je, unalo tatizo la kipanda uso (Migraine), dalili zako ni zipi na ni vitu gani ukitumia unapata nafuu?








Eczema (atopic dermatitis) ni ugonjwa wa ngozi ,unaofanya ngozi kuwasha sana kuwa kavu na kupata vijipele vidogo vidogo vyenye rangi nyekundu,huu ugonjwa ushambulia watoto na wakubwa sehemu za viungo vya mwili (joints) mkononi

Shingoni na miguuni na inaweza tokezea sehemu ya usoni ,juu ya jicho ,makwapani,mgongoni ,tumboni ,mbele ya kichwa (forehead),mapajani,mdomoni na mashavuni. Watoto walio chini ya miaka 5 huwa adhiri kwa asilimia 15% unaweza chukua mda kupona kulingana na ngozi na kiasi cha mtoto alivyoadhirika.

Chanzo cha ugonjwa wa eczema

Eczema inasababishwa na mwili kushindwa kutengeneza au kuzalisha ceramider ,ceramider ni fatty cell inayotumika kwenye uzalishwaji wa ngozi,ceramider inaposhindwa kuzalishwa ngozi ya mtoto inapoteza kiwango cha maji na kuifanya kuwa kavu na ndipo inapo msababishia kuanza kujikuna ,ngozi kuwa kavu na kubadilika rangi kuwa nyekundu.

Eczema ni ugonjwa wa kuridhi -toka kwa mama / baba aliekuwa na ugonjwa ni rahisi mtoto akaridhi.

Mzingo(Allergy au asthma)na pumu huleta eczema

Mtoto anaweza pata allergy ya vyakula tofauti kama maziwa,mayai,ngano,soya samaki,nyaman.k na baadae kumpelekea kupata eczema.

Nini kinachochea kutokupona eczema haraka kwa mtoto

Mtoto mwenye tatizo la eczema anatakiwa aepushwe

Ngozi kuwa kavu (dry skin)-epuka ngozi ya mtoto kuwa kavu itasababisha kuwa na low humidity na kujikuna sana .

Joto kali-joto linapokuwa kali inamsababisha mtoto kujikuna zaidi ,usimveshe mtoto nguo nyingi kipindi cha joto itamfanya ajikune sana .

Food allergy-kuna baadhi ya vyakula vyenye kuleta allergy inatakiwa asipewe kama maziwa,mtindi,mayai,cheese ,nuts(karanga,korosho nk)mikate,pweza,kamba

Acid fruits-matunda ya acid asitumie ndimu ,machungwa,nyanya,strawbell

Acha kutumia vitu vya harufu kali kama sabuni ,perfumes ,majani,na mafuta kwenye mwili wake na nguo zake

Kuogeshwa kwa mda mrefu-epuka kumwogesha kwa mda mrefu au kukaa ndani ya maji isizidi dakika 10 maji yana sababisha ngozi kuwa kavu zaidi,atumie maji vugu vugu wakati wa kumwogesha tumia sabuni ya (sensitive skin) isiyo na harufu na usitumie shampoo

Nguo za kumbana-usimveshe nguo za kumbana au zenye material ya synthetic fabric, wool, ,mveshe nguo za kupwaya ziwe material ya cotton inamfanya ajisikie vizuri bila miwasho.

Nguo mpya-nguo mpya inamfanya ajikune zaidi ,kabla ujamvesha fua kwanza.

Sabuni ya kufulia nguo -nayo inaweza msabishia kuwashwa zaidi ,fatilia kila ufuapo kama ukimvesha izo nguo na kuwashwa sana ujue iyo sabuni haimfai

Kucha kuwa ndefu-zitamkwarua na kujikuna sana kuharibu ngozi zaidi ,hakikisha kucha zake ni fupi kila mara.

Kutompa daily products zozote zitokanaza na ng’ombe au kuku (maziwa,mtindi,mayai,cheesen.k)

Vizuri umpeleke hospital Kupima allergy ili ujue , kama anayo ni rahisi kumwachisha kumpa vyakula vinavyompa allergy mapema kabla hajawa eczema.

Tiba

Eczema kutibika kwa haraka ni ngumu ,kuna dawa za kupaka na ikapunguza muwasho, fatilia masharti hayo nilioandika hapo juu na kula matunda na mboga mboga kwa wingi

Yanayoweza tibu au punguza eczema kwa kiasi kama parachichi ,ndizi mbivu, papai,apple,juice ya carrots ,tango,aloe vera,spinanch ,viazi vitamu,viazi ulaya,smoothie ya tango,parsley.Broccoli na tangawizi unaweza saga pamoja na kumpa mtoto ila kwa wale walio juu ya miezi 6 na kuendelea.

Samaki wa maji baridi kama salmon wanafaa zaidi wana omega 3 ya kutosha.Mwepushe mtoto kula fast food zinachochea ugonjwa kuongezeka

Tiba ya kutibu haya Maradhi ipo kwamtu mwenye kutaka unaweza kunitafuta kwa wakati wako.

Ukiwa na Shida yoyote ile

Usipo pona kwa Dawa za Hospitali nitafute mimi nipate kukutibia upate kupona ukinihitaji matibabu yangu

Unaweza kunitafuta kwa Mawasiliano Herbalist Dr. MziziMkavu What's App +447459370172


 



MKRdezign

{facebook#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {twitter#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {google-plus#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {youtube#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {instagram#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL}

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget