YAFAHAMU MATIBABU YA UKOSEFU WA MAZIWA BAADA YA KUJIFUNGUA. I Dr.Kimario

Baada ya kujifungua, baadhi ya akina mama hutoa maziwa kidogo sana kwa ajili ya watoto wao na wengine hukosa kabisa maziwa.
Hali hii huleta changamoto kubwa kwani mtoto huanza kulia sana na wakati mwingine kuishiwa maji mwilini na kuchemka.
Kitaalamu baada ya kujifungua homoni nyingi za uzazi zinapungua kisha homoni zingine kwa ajili ya uzalishaji wa maziwa kitaalamu kama prolactin hutengenezwa, sasa kuchelewa kwa kwa hatua hii kunaweza kuleta shida hii.


mambo gani unaweza kufanya kutibu tatizo hili?
usiishiwe na maji mwilini: hakikisha unakunywa maji ya kutosha angalau glass nane kwa siku ili kuongeza kiasi cha maji mwilini mwako.
kumbuka maziwa yako kwenye mfumo wa kimiminika hivyo maji mengi yanahitajika kuyatoa.
kula mlo kamili; ungeza ulaji wako wa zamani kwa zaidi kidogo, vyakula vya protini kama mayai, nyama,maziwa nay ng'ombe samaki na mboga za majani husaidia sana sana kuzalisha maziwa ya kutosha ambayo yanaweza kukidhi mahitaji ya mtoto.
tumia virutubisho; taasisi  nyingi za kiafya zinashauri matumizi ya madini ya clacium, vitamin D, Iron, na folic acid kama kiungo muhimu sana katika kumuandaa mama kuzalisha maziwa mengi na yenye virutubisho vya kutosha ndani yake.
nyonyesha mara kwa mara; hata kama maziwa ni kidogo sana jitahidi kumnyonyesha mtoto mara nyingi sana iwezekanavyo yaani mara 10 mpaka 12 ndani ya saa 24 au kila anapohitahi na hii itasaidia sana kutengeneza homoni ya oxytocin ambayo husaidia sana kutengeneza maziwa.
nyonyesha ziwa moja moja; ukimpa mtoto ziwa moja mpaka maziwa yakaaisha kabisa, taarifa hutumwa kwenye ubongo kwamba maziwa yameisha kabisa hivyo ziwa lingine litajazwa maziwa haraka wakati mtoto anamalizia kunyonya ziwa lingine.
matumizi ya dawa; wakati mwingine baadhi ya dawa hutumika hasa pale kiwango cha homoni inayohusika na maziwa inapoenekana iko chini sana na haiwezi kuongeza kiwango cha maziwa.
dawa ya dompiredone huweza kutumika kwa dozi ya 10mg kutwa mara nne na kuongeza mpaka kiwango cha mwisho cha 20mg kutwa mara nne.
Mama anaweza kupunguza dozi na kuacha kabisa kama maziwa yakipatikana, ila ikitokea maziwa yanapungua tena basi ataanza dozi na kuendelea nayo mpaka atakapomuanzishia mtoto vyakula vingine, mara nyingi baada ya miezi sita.
mwisho; wakati mwingine mama anaweza asipate nafuu pamoja nakutumia dawa zote, huenda sababu ya vyanzo vingine ambavyo vinakua nje ya matibabu kama historia ya upasuaji wa matiti na kadhalika hivyo anaweza kutumia maziwa mbadala ya lactogen au maziwa ya ng'ombe .
Labels:

Post a Comment

[blogger][facebook][disqus]

MKRdezign

{facebook#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {twitter#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {google-plus#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {youtube#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {instagram#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL}

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget