KUOSHA SEHEMU ZA SIRI BAADA YA TENDO LA NDOA HUONGEZA MAAMBUKIZI YA UKIMWI.(TAFITI) I Dr.Kimario

Kwa miaka mingi imekua ikifahamika kwamba kuosha sehemu za siri baada ya tendo la ndoa kuna zuia magonjwa ya zinaa kama kaswende, pangusa na mengine ambayo huambukizwa kwa tendo la ndoa, hii imekua ni kweli kwasababu magonjwa ya aina hiyo huhitaji muda wa kutosha kuweza kuanzisha makoloni yao sehemu za siri ili kuleta ugonjwa.
hivyo maji maji yenye ugonjwa huo yakishaoshwa yanasimamisha mfumo mzima wa kuanzisha ugonjwa husika.



Lakini hii imeonekana ni tofauti linapokuja swala la virusi vya  ukimwi kwani kuosha sehemu za siri hasa kwa wanawake na wanaume ambao hawajatahiriwa kumeonekana kuongeza maambukizi badala ya kupunguza.
Utafiti huu ulifanyika nchini Uganda ulichukua wanaume ambao hawajatahiriwa ambao wanatabia hiyo kisha kuchukua wanaume ambao hawana tabia hiyo na kuwafuatilia kwa muda Fulani( cohort studies) na majibu yakionyesha kuongezeka kwa maambukizi kwa 2.3% kwa wale wenye tabia ya kuosha uume wao muda mfupi tu baada ya tendo la ndoa.
Lakini utafiti mwingine ulifanyika nchini kenya kwa muda wa miaka kumi kwa wanawake 1270 na majibu yalionyesha kuongezeka kwa maambukizi ya ukimwi kwa asilimia 2.6% kwa wale walio osha sehemu zao za siri pale pale ukilinganisha na wale waliochelewa na kuosha baada ya dakika kumi mpaka 20.

je chanzo cha maambukizi haya ni nini?
Hakuna majibu ya uhakika wa swali hili lakini wataalamu wamekuja na ababu ambazo huenda ndio zinachangia kutokea kwa jambo hili kama ifuatavyo.
kuongeza ukali wa virusi; sehemu za siri za mwanamke zina maji maji ambayo yana tindikali ambayo kazi yake ni kuua wadudu ambao wanaingia ndani ya uke, sasa ukimwaga maji pale ile tidikali inaishiwa nguvu na kuwapa virusi wale nguvu.
kuongeza michubuko; baadhi ya watu huosha na sabuni au dawa mbalimbali,yale maumivu kidogo unayosikai baada ya kumwaga maji au kupaka sabuni ni kuongezeka kwa michubuko ambayo inatoa nafasi zaidi kwa virusi vya ukimwi kufanya mashambulizi.
kuvipa virusi uwezo wa kuishi na kusafiri; kwa kawaida virusi huishiwa nguvu au kufa pale maji maji yanayovizunguka yanapokauka, kuosha na maji na kuongeza maji maji na kuvihamisha sehemu zingine za sehemu za siri ambazo huenda zina michubuko Zaidi.
mwisho;Kwa lugha nyingine sio vizuri kuosha sehemu za siri muda mfupi tu baada ya tendo la ndoa, jipe muda wa kutosha kitandani na mtu wako kama dakika 10 au 20 ukiwa umepumzika au unafanya mambo mengine kisha unaweza kwenda kunawa.
Labels:

Post a Comment

[blogger][facebook][disqus]

MKRdezign

{facebook#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {twitter#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {google-plus#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {youtube#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {instagram#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL}

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget